Featured Post

HALMASHAURI KALIUA YATOA MIKOPO SHILINGI MILIONI 240

MATANGAZO

Thursday, August 13, 2020

WETCU LTD YAHAMASISHA KILIMO BORA CHA TUMBAKU TABORA


 


Na Allan Ntana, Tabora


CHAMA Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Tumbaku Mkoani Tabora (WETCU LTD) kimeshika nafasi ya kwanza katika Maonesho ya Wakulima Nane Nane Kanda ya Magharibi mwaka huu na kutunukiwa cheti maalumu kwa umahiri wake wa kuhamasisha kilimo bora na kutafuta masoko ya wakulima.


Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake Meneja Mkuu wa Chama hicho Samwel Jokeya alisema kuwa wao kama wasimamizi wakuu wa wakulima wa tumbaku katika eneo lao wana dhamana kubwa ya kuhakikisha zao hilo linawanufaisha wakulima.


Alisema kuwa katika maonesho ya mwaka huu walijidhatiti vya kutosha kutoa elimu stahiki kwa wakulima na kufafanua hatua kwa hatua nini wanachopaswa kufanya ili kilimo hicho kilete tija kiuchumi ikiwemo upatikanaji wa pembejeo.


Alibainisha kuwa banda lao lililopo kwenye uwanja wa maonesho hayo ya Kanda ya Magharibi lilikidhi mahitaji yote ya wakulima na lilionesha uhalisia wa shughuli zote zinazopaswa kufanywa na mkulima ili kumwongezea uzalishaji.


Jokeya aliwataka kuzingatia kanuni, taratibu na maelekezo yote waliyopewa na wataalamu na kuyafanyia kazi ili kuboresha kilimo chao na kuhakikisha kinawainuka kiuchumi.


Mwenyekiti wa Bodi ya Chama hicho Mrisho Rashid Simba alifafanua kuwa jukumu kubwa la WETCU LTD ni kuboresha shughuli za wakulima, kuhakikisha wanapata pembejeo kwa wakati na kuimarisha uhai wa vyama vya msingi.


Alitaja majukumu mengine kuwa ni kupambana na mfumuko wa masoko, kuzuia watoroshaji wa tumbaku, kutafuta makampuni (wanunuzi) wapya ambapo alibainisha kuwa juhudi zao zimewezesha kupatikana kwa wanunuzi wapya ambao ni kampuni ya Grant Tobacco Ltd (GTL), Pach-tech Ltd (PCL) na Magefa.


Ili kumaliza kero ya upatikanaji pembejeo kwa wakati alishauri makisio kufanyika mapema na mzabuni kuhakikisha anakuwa na mawakala wa usambazaji pembejeo hizo kwenye mikoa yote.


Akifafanua sababu za Kampuni hiyo kuibuka kidedea katika maonesho hayo kwa miaka 2 mfululizo kwa sekta zisizo za kiserikali, Kaimu Meneja Shughuli wa Kampuni hiyo Lazaro Abel alisema kuwa ushindi huo umechochewa na dhamira njema waliyonayo kwa wakulima.


No comments:

Post a Comment