Featured Post

HALMASHAURI KALIUA YATOA MIKOPO SHILINGI MILIONI 240

MATANGAZO

Sunday, May 2, 2021

UJUMBE KUTOKA KWA BALOZI WA SWEDEN TANZANIA KWA UMOJA WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI MIKOA YOTE TANZANIA TAREHE 3 MEI 2021



Habari za leo, Mimi kama Balozi wa Sweden ninafurahi kuwepo leo kusherekea uhuru wa habari na kujieleza. Sweden na Tanzania ni marafiki wa siku nyingi, na wote tunatambua kwamba nguzo hii, sambamba na haki ya kupata taarifa ni muhimu sana kwa jamii inayoheshimu Demokrasia na Haki za Binadamu. Sweden inaamini kwamba maendeleo ya nchi yoyote ile yanapatikana kwa kupeana tarifa, kujadiliana kwa uwazi, na kuwajibishana. Basi sisi tutaendelea kuungana na watanzania wote katika jitihada za kukuza na kuendeleza uhuru wa habari na kujieleza nchini. Asanteni sana kwa kunisikiliza 

Saturday, May 1, 2021

WAKULIMA WA TUMBAKU KAHAMA WATARAJIA KUJIPATIA BILION AROBAINI

Wakulima wa Tumbaku wa wilaya ya Kahama wamekuwa wa kwanza kufungua milango ya soko la kuuza tumbaku yao kwenye makampuni  huko mjini Tabora huku wakitarajia kupata zaidi ya shilingi Bilion arobaini kutokana na mauzo ya zao hilo kwa kilo milioni tisa walizoingia mkataba na Makampuni yanayonunua Tumbaku nchini.