Featured Post

HALMASHAURI KALIUA YATOA MIKOPO SHILINGI MILIONI 240

MATANGAZO

Saturday, June 27, 2020

BAKWATA TABORA WAFANYA UCHAGUZI WA DEMOKRASIA SURA MPYA ZAJITOKEZA

TABORA YAJIPANGA VITA DHIDI YA UKATILI WANAWAKE NA WATOTO

TABORA YAJIPANGA VITA DHIDI YA UKATILI WANAWAKE NA WATOTO



 

Mkoa wa Tabora umejipanga kuhakikisha unatokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto ili waweze kuishi kwa kutimiza malengo yao kuondokana na kunyanyaswa na kuonewa.

Wednesday, June 24, 2020

TUMBAKU ILIYOKUWA ICHOMWE MOTO KUWAFUTA JASHO WAKULIMA

Wafanyakazi Mjini Urambo,wakipakia magunia ya tumbaku ambayo ilikuwa ichomwe moto na bodi ya tumbaku ambayo kwa akutochomwa moto sasa itawaingizia wakulima zaidi ya Sh2.3bilioni.
picha na Robert Conrad.


Robert Conrad,Tabora.
Tabora.Bodi ya tumbaku nchini,TTB,imefanikisha kununuliwa tumbaku iliyozidi makisio ambayo ilipaswa kuchomwa moto kutokana na kutokuwa katika hali nzuri huku ikiwa na wadudu na hivyo kufanya wakulima kupata zaidi ya Sh2.3bilioni ambazo wasingezipata kama tumbaku hiyo ingechomwa moto.
Akizungumzia kuhusu suala hilo,kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Tumbaku nchini,TTB,Stan Mnozya,alisema,Tumbaku hiyo inanunuliwa na Kampuni ya Alliance One baada ya mazungumzo na bodi ya Tumbaku,ambapo kiasi cha zaidi ya kilo milioni moja na nusu zenye thamani ya Sh2.3bilioni zitalipwa ,pesa ambazo  kama Bodi ingetumia sheria wakulima wasingezipata.
"Kutokana na hali ya tumbaku ilivyokuwa na kwa kufuata sheria na kanuni zetu ilikuwa tumbaku hiyo tuichome moto lakini wakulima watu wangepoteza kiasi hicho cha pesa"Alisema
Mnozya aliongeza kuwa tumbaku hiyo ilikuwa ni miongoni mwa kilo 12.8milioni zilizozidi makisio msimu uliopita lakini waliweza kuzishawishi kampuni za ununuzi wa tumbaku kuzinunua ingawa kwa bei ya chini na kubaki kiasi cha kilo milioni 1.8 ambazo ndio hizo zilianza kuharibika na zingine kuingiliwa na wadudu.
Alisema kampuni hiyo itawekea dawa tumbaku hiyo na kwamba wanainunua kwa bei ya US Dola 0.58 wastani kwa kilo ambazo angalau wakulima watapata kuliko kukosa kabisa.
kuhusu wakulima ambao tumbkau iliyozidi makisio ilinunuliwa na kampuni moja kutoka nje ambayo haikuwalipa kutokana na tatizo la ugonjwa wa corona,alisema kuwa nao kama kampuni hiyo haitawalipa watalipwa.
Alieleza kuwa kampuni hiyo,viongozi wake walizuiliwa nje ya nchi kutokana na zuio la ugonjwa wa corona na hivyo kushindwa kumalizia mchakato wa kuwalipa wakulima baada ya kununua tumbaku yao iliyozidi makisio.
"Tutatumia mwanya huu kuhakikisha wakulima ambao tumbaku yao ilikuwa inunuliwe na kampuni hiyo,wanalipwa kwani hii iliyobaki inanunuliwa yote"Alisema
Wakulima walisema wanaishukuru bodi ya tumbaku kwa kuwahangaikia na angalau kupata kiasi hicho cha pesa kwani hawakuwa na matumaini kabisa ya kupata angalau kidogo.
"Nitatumia pesa nitakazolipwa kwa kuweka maisha yangu vizuri hasa kipindi hiki cha ugonjwa wa corona unaosumbua duniani na nchini kwetu"Alisema Erasto Mahona mkulima wa Urambo
Naye Jaffary Kankila,alieleza kuwa changamoto ya masomo kwa wanafunzi iliyopo,atatumia pesa atakayolipwa kuhakikisha wanafunzi wanapata vifaa vya kujifunza ili warudipo shuleni wawe vizuri kimasomo.
Kutokana na mauzo hayo ,watakaonufaika sio wakulima pekee bali hata vyama vya msingi kumi na tatu vitakavyopata Sh80milioni na halmashauri ya wilaya ya Urambo itakayojipatia Sh70milioni huku chama kikuu cha Milambo nacho kikitarajia kuingiza Sh34milioni.
Ununuzi wa tumbaku hiyo iliyobaki ambayo kutokana na kukaa muda mrefu ilianza kuharibika na nyingine kuingiliwa na wadudu,kunawapa unafuu wakulima ambao muda wowote mwezi huu wataanza kuuza tumbaku yao waliyovuna.



KAMUSI LUGHA YA ALAMA MBIONI KUKAMILIKA HAPA NCHINI

Tuesday, June 16, 2020

DED KALIUA ATOA MOTISHA KWA WALIMU SHULE YA MSINGI UGANSA



Na Allan Ntana, Tabora                                                                        
MKURUGENZI Mtendaji wa halmshauri ya wilaya ya Kaliua Mkoani Tabora Dkt John Marco Pima ametoa motisha ya fedha taslimu zaidi ya sh 160,000 kwa walimu wa shule ya msingi Ugansa iliyoko katika kata ya Usinge kwa kufaulisha wanafunzi wote.

Akizungumza na mwandishi wetu, Dkt Pima alisema kuwa motisha hiyo imetolewa hivi karibuni kama pongezi kwa walimu wa shule hiyo baada ya kuiwezesha kuwa ya kwanza kiwilaya kwa miaka 2 mfululizo katika matokeo ya darasa la saba.

Aliongeza kuwa juhudi kubwa zilizooneshwa na walimu hao wakiongozwa na Mwalimu Mkuu Cosmas Seleka Leonard zimewezesha watoto wote waliomaliza darasa la saba 2018 na 2019 kuchaguliwa kujiunga na shule za sekondari.

Dkt Pima alieleza kuwa utendaji wa walimu wa shule hiyo ni mfano wa kuigwa na shule nyingine na kuahidi kuendelea kuwapa motisha, kwani licha ya kuwa kijijini imeshika nafasi ya 6 kimkoa na kushindana na shule za mchepuo wa kingereza.

‘Nimetoa motisha ya sh 100,000 kwa ajili ya shule, nimetoa zaidi ya sh 50,000 kwa idadi ya alama ‘A’ za kila somo ambazo mwalimu wa somo husika alipata na sh 50,000 kama motisha kwa uongozi wa shule’, alisema.

Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Cosmas Seleka alifafanua kuwa mwaka 2018 wahitimu wa darasa la 7 katika shule hiyo walikuwa 78 na mwaka 2019 walikuwa 70 na wote walifaulu mitihani yao ya mwisho na kujiunga na shule za sekondari.

Aidha alimshukuru Mkurugenzi kwa kutoa zawadi kwa walimu wote waliofaulisha kwa kiwango cha ‘A’ katika somo lolote ambapo kila A alitoa sh 500/- , walimu zaidi ya 15 walijipatia kifuta jasho cha fedha taslimu kulingana na idadi ya A zilizopatikana kwenye somo lake.

Akilezea siri ya mafanikio hayo, Mwalimu wa Taaluma shuleni hapo Mwalimu Malundi Stefano Malundi alisema kuwa ushirikiano wa dhati baina ya walimu na usimamizi madhubuti wa ratiba ya vipindi vya darasani ndio siri ya matokeo hayo.

Aliongeza kuwa walimu wote wanajali sana muda kwani wanaamka saa 11 alfajiri na kujiandaa na kila siku vipindi vinaanza saa 1.00 asubuhi na watoto wanakaa shuleni hadi saa12.00 jioni wakiwa na walimu wao.

WAGANGA TIBA ASILIA WATAKIWA KUWA WABUNIFU

Wazee  wa  Kimila  na  Waganga  wa Tiba  mbadala  wilayani Kaliua mkoani Tabora


Na Allan Ntana, Tabora

WAGANGA wa tiba asilia wilayani Kaliua Mkoani Tabora wameshauriwa kuongeza ubunifu katika utoaji huduma za tiba mbadala ili kuisaidia serikali katika kukabiliana na magonjwa hatarishi ya mlipuko ikiwemo ugonjwa wa corona.

Ushauri huo umetolewa jana na Ofisa Tarafa wa tarafa ya Kaliua Bethord Mahenge alipokuwa akifungua mkutano wa Chama cha Wazee wa Kimila wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo Abel Busalama.

Aliwataka Wazee wa Kimila kwa kushirikiana na Waganga wa tiba asilia kuendelea kubuni tiba mbadala zitakazosaidia kukabiliana na magonjwa yasiyo na dawa kama vile ukimwi na homa kali ya mapafu (covid 19).

Alisisitiza kuwa dawa za asili ni tiba mbadala yenye uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa mbalimbali miongoni mwa jamii, tatizo lililopo ni kukosa ubunifu kwa wahusika na wengine kuingiza ujanja ujanja usiokuwa na tija kwa jamii.

Mahenge alibainisha kuwa baadhi ya waganga wamekuwa sio waadilifu katika kazi zao na wengine wamekuwa sio wa kweli jambo linalopelekea kutoaminika kwa huduma wanazotoa miongoni mwa jamii.

‘Ndugu zangu tuache tamaa ya fedha katika kutekeleza wajibu wetu, tusaidie jamii kwa moyo wa dhati, toeni taarifa za wale wanaoendekeza ulaghai na kuwaibia wananchi ili wasiendelee kuchafua chama chenu’, alisema.

Mahenge alitoa wito kwa waganga wa tiba asilia na wazee wa kimila kumtanguliza Mwenyezi Mungu katika kazi zao na kuwa marafiki wa serikali kwa kufichua wahalifu na kukomesha vitendo hivyo miongoni mwa jamii.

Ili kukomesha tabia za ulaghai miongoni mwao aliwataka kuhakikisha kila mmoja anajiandikisha ili ijulikane anakoishi na uongozi wa chama hicho umtambue ili atakapopata matatizo aweze kupata msaada.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Mwanahamisi Juma alipongeza Chama cha Wazee wa Kimila wilayani humo kwa mwamko wao wenye dhamira ya kukomesha na vitendo vya unyanyapaa kwa watoto na akinamama.

 Ili kufanikisha majukumu yao ya kila siku aliwataka kufuata sheria, kanuni na taratibu na kujiepusha na ramli chonganishi kwa kuwa zinaongeza uhasama na chuki miongoni mwa jamii.